Monday, November 4, 2013

Uvimbe sehemu ya haja kubwa - bawasiri/bawasili (HEMORRHOIDS)

Bawasiri ni mojawapo ya tatizo ambalo mara nyingi linapotokea humfanya mtu kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba sahihi. Bawasiri au hemorrhoids husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.

Kuna aina mbili za Bawasiri

Nje: Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa, na huweza kuambatana na maumivu, pamoja na kuwashwa kwa ngozi katika eneo hilo. Mara nyingine mishipa hiyo ya damu (vena) hupasuka na damu huganda na kusababisha aina kitaalamu inaitwa Thrombosed hemorrhoid.

Ndani: Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa. Na huwa haimbatani na maumivu na wengi huwa hawatambui kuwa wanatatizo hili.

Aina hii imegawanyika katika mainisho yafuatayo:
  • Daraja I- Bawasiri kutotoka katika mahali pake pa kawaida
  • Daraja II- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya tukio hilo.
  • Daraja III- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kuirudisha mwenyewe baada ya tukio hilo.
  • Daraja IV- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na vigumu mtu kuirudisha baada ya tukio hilo.
Je bawasiri husababishwa na nini?

Bawasiri husababishwa na;
  • Tatizo sugu la kuharisha
  • Kupata kinyesi kigumu
  • Ujauzito
  • Uzito kupita kiasi (obesity)
  • Kupenda kufanya ngono ya njia ya haja kubwa (anal sex)
  • Kwa ujumla mambo yanayo ongeza shiniko katika tumbo.
  • Umri mkubwa
Dalili za bawasiri
  • Damu kunuka kinyesi wakati wa kujisaidia (hematochezia)
  • Maumivu au usumbufu
  • Kinyesi kuvuja
  • Kijiuvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
  • Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
  • Kujitokeza kwa kinyama (bawasiri) wakati wa haja kubwa
Matatizo yanayoweza kutokana na Bawasiri
  • Upungufu wa damu mwilini (Anemia)
  • Strangulated hemorrhoids
Vipimo na uchunguzi
  • Digital rectal examination
  • Kipimo cha njia ya haja kubwa (Proctoscope)
  • Kipimo cha utumbo mpana (Sigmoidoscope)
Matibabu

Matibabu hutegemea na hali na aina ya Bawasiri
  • Rubber band ligation - Hapa mishipa hufungwa na rubber band ili kuzuia damu kwenda kwenye eneo liloathirika, na hutumika kwenye aina ya ndani ya bawasiri.
  • Sclerotherapy- Hapa kemikali huwekwa kwa njia ya sindano
  • Coagulation (infrared, laser and bipolar)
Upasuaji;
  • Hemorrhoidectomy
  • Stapled hemorrhoidopexy
Njia za kuzuia Bawasiri
  • High fibre diet, kula mboga za majani, matunda, na nafaka kwa wingi.
  • Kunywa maji mengi kwa siku (glasi sita had nane kwa siku)
  • Punguza kukaa kwa muda mrefu sana hasa ukiwa chooni, kwa sababu unaweza kuongeza shinikizo katika mfereji wa haja kubwa.
...........................................................................................
Kuota kinyama njia ya haja kubwa

Unasumbuliwa na Kitu kinachoitwa HEMORRHOIDS na bawasili ni neno fasaha la kiswahili!bawasili inasababishwa na kupata Choo kigumu kwa muda mrefu mpaka kusababisha mishipa ya damu kutanuka kwasababu haiwi emptyed ipasavyo!hio ACOSAL ANAL ointment ni dawa sahihi kabisa au SCHERIPROCT ambayo Ina prednisolon!kama hizo dawa Njia pekee ilobakia ni upasuaji!

1. Jaribu kunywa maji ya kutosha na kula chakula chenye fiber nyingi ili uepuke kupata Choo kigumu.
2. Epuka kusimama muda mrefu au kukaa muda mrefu kama ulikuwa unafanya hivo awali
3. Fanya mazoezi ili kuongeza intenstine motility
4. Epuka kujikamua sana ukipatwa na haja kubwa

NB: Huu ugonjwa hahuhusiani na matatizo ya uzazi
......................................................................................

Haemorrhoids ni uvimbe ambao unaweza kutokea katika njia ya haja kubwa (------) na sehemu ya mwisho ya puru (rectum).
 
Kuna mtandao wa veins ndogo (mishipa ya damu) inayopita ndani ya ------ na sehemu ya chini ya rectum. Hizi veins mara nyingine zinakuwa pana na kujaa damu zaidi kuliko kawaida. Mishipa hii iliyoja damu pamoja na tishu zilizojuu yake inaweza kufanya uvimbe mmoja au zaidi uitwao haemorrhoid.

Sababu halisi kwa nini mabadiliko haya hutokea na kusababisha haemorrhoids hazijulikani. Hata hivyo, inadhaniwa kwamba shinikizo (pressure) katika ama karibu na ------ inaweza kuwa sababu kubwa katika kesi nyingi. Kama shinikizo katika ama karibu na ------ limeongezeka, basi ni wazi kwamba hii inaweza kusababisha haemorrhoids kutokea

Baadhi ya sababu zinazopelekea hali hiyo ni

-kufunga choo ama kupata choo ngumu 
-ujauzito
-sababu za kiurithi-baadhi ya watu wanaweza kuwa na kuta dhaifu

Dalili

Dalili zinaweza kutofautiana. Haemorrhoids ndogo kwa kawaida haina maumivu. Dalili ya kawaida ni kutoka damu baada ya kwenda choo. Haemorrhoids kubwa huweza kutokwa majimaji kama makamasi, maumivu kiasi, kuwasha, na kujikuna. Unaweza kuwa na hisia za haja kubwa , au hisia ya kuwa bado unahitaji kwenda haja kubwa hata baada ya kujisaidia.Wakati mwingine damu huganda kwenye haemorrhoids na hivyo huleta maumivu makali. Maumimu haya hudumu kwa siku kadhaa lakini baadae hukoma.

Matibabu

Hakikisha unapata choo la laini wakati hivyo unaweza kufanya yafuatayo.

-Kunywa maji mengi
-kula vyakula vyenye nyuzinyuzi kwa wingi mfano matunda mboga za majani na vyakula vya nafaka.
-Epuka dawa za maumivu zenye codaine mfano
-Nenda chooni mara tu unapohisi haja.Usijaribu kubana.

Njia hizo zote hapo juu zitasaidia kupunguza dalili mfano damu kuacha kuvuja.
Hata hivyo kuna dawa nyingine ambazo unaweza kupaka amu kuingiza kwenye ------. Dawa hizi hazimalizi tatizo bali husaidia kupunguza dalili.
Matibabu mengine ni upasuaji ambayo inaweza kuwa kufunga (banding) au kuondolewa (haemorrhoidectomy).


2 comments:

  1. iyo bawa siri inamazala gani makubwa

    ReplyDelete
  2. Yani nimevurugwa nimekaona katoto kangu ka miaka 5 kwa nje juu kanyama keupe hivi ila hajalalamika, sasa madhara yake ninini?

    ReplyDelete